1
DOGO: Eti mama malaika huwa wanapaa?
MAMA: Ndio malaika wanapaa, kwanini unauliza?
DOGO:Baba alimuita dada Malaika, dada atapaa?
MAMA: Ndio atapaa leoleo kurudi kijijini kwao
2
GULO: Bebi simu yako nzuri umepata wapi?
DEVI: Nilishinda kwenye mashindano
GULO: Mashindano ya nini Bebi?
DEVI: Mashindano ya mbio, kati yangu, mwenye simu, polisi na wananchi wenye hasira kali.
No comments:
Post a Comment
SEMA USIKIKE