24 January 2013

MPENZI WANGU TOKA UVUNGUNI

Jamaa karudi home ghafla na kupata mshtuko kukuta mkewe mpenzi ana bwana ndani, baada ya zogo kubwa, wanaume wakaenda ukumbini kumalizana kiungwana;
MUME: Sikiliza mi nakusamehe niachie mke wangu ananipenda ila ni shetani tu kampitia
MGONI: Lakini mimi niko nae siku nyingi, hawezi kuniacha ananipenda sana
MUME: Hebu tufyatue risasi na kujifanya tumeuwana atakayeliliwa zaidi achukue mke....wakafyatua risasi mke akaja mbio akipiga kelele na kukuta wanaume wamelala chini......akaanza kucheka na kurudi chumbani
MKE: Mpenzi wangu toka huko uvunguni wale mafala wamejipiga risasi wamekufa wote

No comments:

Post a Comment

SEMA USIKIKE