1. Na ikatokea katika zama za utawala wa awamu ya 4,
mara baada ya lile apizo la kuingia katika dijitali, muda mfupi baada ya watu wa kule mbali kuamua kutimiza yale yaliyosemwa toka kale za mababu zao, kuwa kila mtu atapumua kwa gesi yake, hapo ndipo binadamu wale, wake kwa waume, wakatokewa
na matatizo makubwa na kuwa watu wa kutoa visingizio, wengine walisema, chaja
yangu iligoma, na wanawali walilalamika kuwa wanaume wa wakati ule hawakutaka
kupokea simu zao, wengine walilalamika kuwa imani yao iliwazuia wasiwasiliane
na wanawali, na wengine walitangaza kuwa wangechukua muda ule kujifungia ndani
na familia zao kwani wanao hawakuwajua wote. Wengine walilalamika kuwa wakubwa zao wa kazi
waliwatuma mbali, wengine walidai mama zao wanaumwa katika vijiji vilivyo mbali,
wengine walidai kuwa mashine za ATM zilimeza kadi zao, wengine walidai magari
yao yaliharibika, wengine wakadai kuwa imani zao ziko katika msimu wa kufunga na
kujitafakari na hivyo si vema kufanya sherehe wala hata kucheka. Wengine walidai wamo katika kazi za kuumbua mafisadi na wangezunguka utawala wote kuhubiri ujio wa zama bila ufisadi. Naam naam
nawambieni Enyi wanadamu mkiona ishara hizi, msifadhaike, bali shangilieni
kwani zinashiria kuwa tarehe 14 ya Februari ikaribu Kitime 29:1
No comments:
Post a Comment
SEMA USIKIKE