15 November 2017

WAHENGA WENZANGU TUHAME MJI MAPEMA

Ndugu wahenga wenzangu, salama macho? Ndege itatua au fitna? Basi tutayafiksi au vipi? Basi doleeee na baada ya salamu naomba niwaambie wazi kuwa hofu nyingi na mashaka juu yenu mliye mbali na upeo wa macho yangu mhenga mwenzenu. Ndugu wahenga, samahani natumia neno ndugu, si mnakumbuka enzi zetu kila mtu alikuwa anaitwa ndugu, tulikuwa hatuitani sijui, oyaa, mshkaji, mkuu, kibosile, mheshimiwa, mtukufu, sisi wote tulikuwa tunaitana ndugu, kwa hiyo ndugu wahenga mambo yamekuwa si mambo tena, sisi wenyewe ndio tulisema ‘asiyekubali kushindwa si mshindani’. Ndugu zangu tukubali tumeshindwa na nashauri tuhame mji tuwaachie wenyewe. Wahenga mambo yamebadilika juu chini, enzi zetu mnakumbuka binti akipata mimba nje ya ndoa alikuwa akijificha kwa aibu na mara nyingine aliweza hata kunywa sumu? Siku hizi binti akipata mimba nje ya ndoa ndio kwanza anapiga picha tumbo analiweka mtandaoni dunia nzima ilione, hajali kama ataliona baba mkwe wake wala baba yake mzazi, yaani we acha tu. Ndugu wahenga mtakumbuka kitu hicho kingetokea enzi zetu mwaka huo hata mvua isingenyesha hapo kijijini na mizimu ingetoa adhabu hapohapo, pengine ukoo wa binti aliyefanya kufuru hiyo ungefukuzwa wote kijijini, a pagelazimika kufaya tambiko la kuchinja ng'ombe dume wawili. 
Siku hizi unaweza kuona mama yake mzazi akisifia kitendo hicho, na kushukuru Mugu kwa binti yake kuwa mjamzito hapo uaanza kusukwa mtego ili aliyempa mimba atolewe upepo, wala sio lazima amuoe, kikubwa aaze kuleta pesa za matunzo.
 Ndugu wahenga mnakumbuka zamani binti wakati anaolewa alikuwa mtu wa aibu tena na machozi yatamtoka kwa uchungu wa kuachana na familia yake? Siku hizi kuolewa kunafanyiwa utani tu, wala wazazi hawataarifiwi, bibi harusi anaruka ruka harusini kuliko hata bwana harusi, yaai mambo yamegeuka uaweza kukuta bwana harusi ndie katulia aaonekana kuwa a mawazo ya jinsi ya kuanza maisha na bibi harusi mapepe.
 Ndugu wahenga mnakumbuka tulivyokuwa tunapishana kistaarabu barabarani wakati tukiendesha baiskeli zetu za foneksi a raleee na magari yakipita barabara hiyohiyo, jaribu leo kupita na baiskeli yako, utagongwa na bajaj, ezi zetu (tunaziita pikipiki za magurudumu matatu) au gari au bodaboda (tulikuwa tuaziita tukutuku au pikipiki) kabla hujafika mbali, na watu wote watakujia juu kwanini unaendesha baiskeli barabarai, sasa baiskeli iaedeshwa shambani?
 Ndugu zangu wahenga, enzi zetu za redio tulikuwa tukisikiliza maneno ya busara na muziki wenye burudani na mafunzo kutoka kwenye redio lakini sasa usishangae matusi ya nguoni yakitajwa na kuambia ndio muziki, na huko kwenye luninga hakuna afadhali, picha  zinaonyesha wajukuu zetu wakijitahidi kushindana kuvaa nguo ndogo zaidi kila siku, eti ndio wimbo utapendwa.
Ndugu zangu wahenga nawaomba tuwaachie hawa mji, tutafute mji mpya huko porini tuanze moja, tuwaachie waendelee kudaiana fidia ya matunzo ya watoto ya mamilioni kwa mwezi. Tuwaachie watoto wa kiume waendelee kuvaa suruali zinazolegezwa makusudi ili makalio yaonekane, sijui ili nani awaone? Tuwaachie mji mabinti wanaojifanya wanaume. Ndugu wahenga tuhame mji, iko siku hawa watatuhamisha kwa nguvu tukubali tumeshashindwa…. 

No comments:

Post a Comment

SEMA USIKIKE